Sifa muhimu za ugonjwa wa akili ni kuvurugukiwa kwa hisia, mawazo au tabia za watu. Jambo ambalo ni nje ya utaratibu uliozoeleka wa imani zao za kitamaduni na nafsi zao. Na upelekea kutokea kwa athari hasi katika maisha yao na familia zao.
Magonjwa ya akili yaliyo kali, yana kawaida ya kuwa sugu kutokea kwa vipindi na sio mfululizo. Na huwa na athari za muda mrefu kuhusu kupungua kwa uwezo wa kutenda mambo.
Magonjwa yanayotokana na matumizi ya mihadarati/pombe yameenea sana katika jamii zetu. Na kwa ujumla yana athari sana kwenye jamii katika uzalishaji, afya na usalama. Pombe inatumika vibaya zaidi katika jamii nyingi za Kitanzania ikifuatiwa na tumbaku na bangi.
Vitu vingine ni pamoja na uvutaji wa vitu vyenye kulevya (petroli, mafuta ya taa, gundi, na kadhalika), miraa na heroini.
* Magonjwa yasiyo ya yakuambukiza kama vile kisukari na magonjwa ya moyo (pombe).
* Magonjwa sugu ya mapafu na saratani za matumbo (tumbaku).
* Tabia zinazohusiana na kuathiriwa na dutu hizi.
* Umiliki wa dutu haramu.
* Hatua zilizochukulikwa kinyume na sheria katika upatikanaji wa dutu hizo pale wahusika wanapokuwa tegemezi.
MUHIMU: Magonjwa ya akili yanatibika, na mengi yanaweza kudhibitiwa katika ngazi ya zahanati. Kwa ushirikiano wa ziada kutoka kwa mtumishi wa afya ya jamii na wanajamii wenyewe kwa ujumla.
